Учебник соответствует разделу 2 (семестры 4-6) действующей обновленной Программы по языку суахили (основному) для студентов факультета международных отношений, уровень "Бакалавр"

Вид материалаУчебник
12. Переведите текст и перескажите его на суахили: Sheikh Abeid Amani Karume
Biashara ya watumwa
Подобный материал:
1   ...   10   11   12   13   14   15   16   17   ...   26

Mazoezi

5. Дайте русские эквиваленты:

mashujaa wenye kusimamia kweli; -thibitisha ushujaa wake; enzi za kikoloni; ingetosha kwake kuitwa mwalimu; -pata shahada ya ualimu; jina lenye sifa na hadhi kubwa; asili ya chama; chombo cha kuunganisha watu; moyo mkunjufu; -jiandikisha katika chuo kikuu; -toa hotuba; mali ziligawanywa kwa hila; -jiuzulu katika kazi; -jizamisha kwenye siasa; matumaini ya mbele; ukweli haukuweza kufichama; -kataa kuajiriwa; mgawo wa wajumbe; -churupuka mikononi mwa adui; -susia uchaguzi; la sivyo; -gombea uchaguzi; -acha kwa hiari; -sita kufanya jambo; mkataba ulikubaliwa rasmi; maneno ya ufidhuli; -weka balozi; -leta dhiki; -apishwa kuwa rais.


6. Дайте эквиваленты на суахили:

выступать за правду; выступать на собрании; выступать вперед; во времена колониального господства; во время каникул; приходить вовремя; преуспеть в учебе; добиться успеха; успешно сдать экзамен; достойное имя; популярное имя; известное имя; человеческое достоинство; средство объединения; орудие борьбы; рабочие инструменты; бороться за независимость; биться с врагом; вести борьбу; уходить в отставку; уходить с поста; уходить из дома; мрачные перспективы; хорошие перспективы; не иметь никаких перспектив; разжигать огонь; разжигать войну; сеять вражду; осуждать кого-либо; обвинять друг друга; обвиняемый; бойкотировать выборы; одержать победу большинством голосов; баллотироваться на выборах; разрывать официальные отношения; устанавливать добрые отношения; развивать отношения.


7. Составьте 10 вопросов на суахили по содержанию текста и дайте на них ответы.


8. Расскажите на суахили, что вы знаете о Дж. Ньерере.


9. Переведите, используя желательно-побудительное наклонение с показателем -ka-:

1. Преподаватель велел нам сходить в библиотеку и взять новые учебники. 2. Мы попросили водителя ехать прямо, затем свернуть налево и остановиться. 3. Исследователь поехал в Индию для того, чтобы изучить жизнь слонов и написать о них книгу. 4. Давайте зайдем в кафе и поедим, так как впереди у нас долгий путь. 5. Соседка попросила меня съездить на вокзал и встретить ее дочь, поскольку сама она заболела. 6. Позвони редактору и скажи ему, что он должен срочно приехать на работу. 7. Если ты не знаешь, как готовить эту рыбу, иди и спроси у повара. 8. Полицейский приказал грабителю бросить свой нож и поднять руки.


10. Переведите текст:

Rashidi M. Kawawa

Rashidi Mfaume Kawawa, ambaye alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika tarehe 22 Januari 1962, alipojiuzulu Julius K. Nyerere, ndiye aliyeanzisha vyama vya wafanya kazi nchini Tanganyika. Alizaliwa mwaka 1930. Alipochaguliwa kushika usukani wa serikali, alikuwa amekwisha fanya kazi za siasa, utumishi wa serikali na kuwa mchezaji hodari katika picha za sinema.

Rashidi Kawawa alizaliwa Songea katika ukoo wa mfanya kazi serikalini na mwindaji mashuhuri. Ukoo mzima wa Kawawa ni wawindaji mashuhuri. Rashidi M. Kawawa alielemishwa katika shule ya sekondari ya serikali, Dar es Salaam, na baadaye katika shule ya sekondari ya serikali, Tabora, ambako alijulikana sana kwa uhodari wake katika michezo ya kuigiza. Rashidi Kawawa alipendelea sana kazi za maendeleo, lakini alipoomba kazi katika Idara hiyo mara ya kwanza, alikataliwa kwani eti alikuwa mdogo mno. Badala yake akaingia kazi ya ukarani katika wizara ya usafirishaji umeme na kazi na baadaye alipata uhamisho kwenda Idara ya maendeleo mwaka 1951.

Rashidi Kawawa alipokuwa mfanya kazi katika Idara ya maendeleo aliendesha sinema na kuangalia maktaba ya picha za sinema – hata baadaye akajulikana sana kama mchezaji maarufu katika picha za sinema za Kiswahili kadha wa kadha. Zaidi ya kazi hizo alikuwa mshauri juu ya jadi za Kiafrika kwa wataalamu wa kutengeneza picha za sinema.

Mwezi Februari 1956, Rashidi Kawawa alijiuzulu katika kazi za serikali na akawa katibu mkuu wa Shirikisho la vyama vya wafanya kazi Tanganyika. Wakati huo huo pia akaaingia TANU. Akiwa katika kazi ya vyama vya wafanya kazi, alitembelea nchi mbali mbali za nje kuhusiana na kazi yake. Katika uchaguzi mkuu mwaka 1960 Rashidi Kawawa aliingia katika Baraza la kutunga sheria bila kupingwa akiwa mjumbe wa Nachingwea.

Rashidi Kawawa aliposhika usukani wa kuendesha nchi, yaani katika kipindi alipokuwa waziri mkuu, mambo mengi yalirekebishwa na serikali ya wananchi: vyama vya ushirika vingi vilianzishwa; utaratibu wa kumiliki ardhi ulitengenezwa ili upatane na mila za wananchi juu ya umilikaji wa ardhi; migomo ilifanywa si njia halali ya wafanya kazi kudai haki zao mpaka idhini ya waziri imetolewa. Shauri la kuitaka Tanganyika iwe Jamhuri lilikatwa kwa vile wananchi wengi walikuwa wanakerwa kerwa na lile jambo la kuwa chini ya malkia wa Waingereza hata baada ya nchi yao kupata uhuru kamili. Kwa upande wa serikali, mwaka 1962 ulikuwa mwaka wa kufanya kazi kweli ili kuipa nchi yetu sura ya Utanganyika. Katika kazi za serikali wananchi wengi walipewa madaraka makubwa sana. Wananchi pia waliitikia kwa kujitolea katika kazi za kujenga taifa.


11. Переведите текст:

Джомо Кениата родился в 1891 году примерно в 50 километрах от Найроби в довольно известной семье. Его отец и дед считались мудрыми людьми, которые могли давать советы и предсказывать будущее. Мальчику дали имя Камау Нгенги. В 1907 году он поступил в миссионерскую школу. Спустя семь лет, Нгенги принял христианство, и ему дали имя Джонстон. Джонстон Камау успешно окончил школу, проявив прекрасные способности и большую любознательность. В 20-е годы он работал переводчиком в Верховном суде, затем поступил на работу в департамент водоснабжения муниципалитета Найроби. “Мои обязанности, – рассказывал Кениата, – заключались в сборе денег за воду. Я носил широкий пояс, который на моем языке называется “кениата”. За этот пояс я закладывал полученные деньги. Когда ехал на велосипеде, мальчишки бежали за мной и кричали: “Кениата! Кениата!” Это слово так привязалось ко мне, что для многих я стал изестен как Кениата. Имя Джонстон впоследствии я заменил на более близкое моему народу – Джомо”. Так появилось имя Джомо Кениата, которое уже в конце 20-х годов стало известно не только в Кении.


12. Переведите текст и перескажите его на суахили:

Sheikh Abeid Amani Karume

Sheikh Abeid alizaliwa Unguja, kijijini Mwera, Wilaya ya Kati, katika mwaka 1905. Alipofika umri wa miaka minane, alipelekwa skuli ya hapo hapo kijijini kwa kusoma. Yeye alikuwa katika wale wanafunzi wa kikundi cha awali kupelekwa hapo na ndio walioifungua shule hiyo iliyojengwa na serikali.

Baba yake alipokufa Abeid alikuwa ni mtoto wa miaka minane tu. Kwa hayo yaliyotokea, aliona skuli nzima ni kama kwamba iliyofunikwa na giza. Pamoja na hayo alijikaza hivyo hivyo kuhudhuria. Ilikuwa ni kawaida yake anaporejea nyumbani kumsaidia mama yake Bibi Amina katika machungaji ya ng’ombe. Pia humsaidia katika kazi nyingine ndogo ndogo za hapo nyumbani kwani yeye akapenda kujituma na kufanya kazi hii na ile.

Alipofika umri wa miaka 13, mama yake mpenzi alimpeleka mjini kuendelea na masomo. Yeye hakuwa mgeni hapo mjini, kwani Mwera ipo masafa ya maili 7 tu kutoka mji mkuu wa Unguja. Kwa vile alivyokuwa akija mjini baadhi ya nyakati, aliweza kujuana na watoto wengi wa makamo yake na kuchanganyika nao katika michezo.

Wakati huo, zilikuwa zikipitia Unguja meli za namna kwa namna, kwani hii ilikuwa ikihesabika kuwa ni moja katika bandari mashuhuri ya Afrika ya Mashariki. Pia zikiteremsha bidhaa za kila aina na kuchukua zile za pande hizi. Nyingi katika meli hizo mpaka hivi leo zinatia nanga bandari hii ya Unguja. Kwa hivyo, hapo pwani zilizuka kazi nyingi na vijana chungu nzima waliweza kujipatia kazi ya kufaa. Abeid naye pia alijitia humo pamoja na wananchi wenziwe. Kwa vile alivyopata fursa ya kuzipandia meli nyingi, kukutana na kuzungumza na wasafiri, mabaharia na wafanya kazi wa humo, ilimjia hapo na yeye hamu kubwa ya kutaka kusafiri, kuona nchi za nje na kuweza kushuhudia kwa macho yake namna mataifa mbali mbali yanavyoishi katika dunia yetu hii.

Mawazo hayo yalimkaa sana moyoni mwake. Hapo alimkabili mama yake mpenzi na kumweleza fikra na maazimio yake na alimtaka ampe ruhusa kwa kuingia katika kazi za bahari. Bibi Amina alimkubalia mwanawe kuwa mwana wa bahari kwa kusikia kuwa safari zake zitakuwa za zile nchi za jirani na ataweza kumwona mwanawe kila mara meli yake itakapofika Unguja.

Katika 1920, Sheikh Abeid alitimia miaka 15 na hapo alipokelewa na kampuni kufanya kazi katika merikebu zao zile zinazosafiria pwanipwani ya Afrika ya Mashariki kwa kuipitia bandari kama zile za Dar es Salaam, Mikindani, Mafia, Tanga, Mombasa na kadhalika. Sheikh Abeid hufurahi sana meli yake inapofika Unguja, kwani hupata fursa ya kumzuru mama yake mpenzi, wazee wengine na kuonana pia na marafiki zake.

Baada ya miaka miwili, Sheikh Abeid katika 1922 aliingia kufanya kazi katika meli za nje na zile zilizosafiria nchi za mbali. Humu ndimo alimopata maarifa mengi na kuziona mwenyewe zile faida nyingi za safari. Katika miaka 17 aliyoipitisha humo merikebuni kwa kufanya kazi za namna mbali mbali, aliweza kuzitembelea nchi nyingi.

Katika mwaka 1938 fikra ilimjia ya kurejea kwao. Aliona wakati umefika kuyatumia yale maarifa aliyoyapata kwa masilaha ya wananchi wenzake. Zama hizo hizo ndipo alipowakusanya mabaharia na wafanya kazi wote wa mashua na motaboti za pwani na kuunda jumuiya yao ya ushirika. Kabla ya kusimamishwa jumuiya hii, wafanya kazi wa hapo wote walikuwa wakilipwa ujira mdogo tu. Mapato yote na mipango yote ya kazi ilikuwa ikidhibitiwa na matajiri wenye kumiliki mashua hizo. Kuwekwa kwa jumuiya hii kuliondosha ubepari huo na badala yake kumeleta faida nyingi. Umeondoka ule mgogoro na chuki; na badala yake yamepatikana masikilizano mazuri baina ya wafanya kazi na matajiri.

Huo ndio ushirika wa kikweli ulioletwa na kiongozi huyo. Msingi huu madhubuti wa ushirika alioujenga hapo pwani ulimpelekea kiongozi huyo kusifika na kupendwa si na wafanya kazi wa hapo tu, bali na wa sehemu nyingine za wananchi wote. Umashuhuri wake katika kujenga msingi wa kitaifa ukaanza kuzungumzwa, kujulikana na kuenea.


13. Дайте синонимы следующим словам и выражениям или объясните их смысл на суахили:

-piga marufuku; -vumbua; -funua; -pasha habari; -pata idhini; -tia mashaka; -teka; mamlaka; -shuhudia; mtemi; -hifadhi; -enda taratibu; -kumpa mtu usia; -kumvamia mtu; -dhoofika; -toroka gerezani; -la kiapo; -toa kauli; -susia uchaguzi; -jinyakulia ushindi; -jiuzulu; vinginevyo; -leta dhiki; -rekebisha; halali; -kera; masafa marefu; mgogoro umezuka; -pewa fursa; madhubuti; -shika usukani wa nchi; -pata uhamisho kazini; -itikia ombi; -tabiri hali ya hewa; mtu wa makamo yangu; merikebu; -zuru, zama za ukoloni; -pata ujira; -dhibiti migogoro ya mabaharia.


14. Переведите:
  1. Дж. Ньерере – один из немногих лидеров Африки, отстаивавших справедливость и человеческое достоинство.
  2. Получив диплом об окончании Университета, он полностью посвятил себя политической борьбе.
  3. Ньерере использовал партию как инструмент объединения народа в борьбе за достижение национальной независимости.
  4. Перед ним стояла задача сформировать партию нового типа, которая смогла бы успешно вести борьбу с колонизаторами.
  5. Ньерере добровольно оставил преподавательскую деятельность и с головой ушел в политику.
  6. Губернатор обвинял его в подстрекательской деятельности и грозил заключить в тюрьму.
  7. Ньерере убедил своих последователей не бойкотировать выборы в Законодательное Собрание.
  8. Кандидаты от ТАНУ участвовали в выборах и одержали победу, получив все места в Национальном Собрании.
  9. Ньерере был тверд в своей решимости защитить национальную независимость.
  10. Танзания была одной из семи стран, разорвавших отношения с Великобританией.
  11. Победив большинством голосов на выборах, Дж. Ньерере был приведен к присяге как первый президент Республики Танзания.


Msamiati

-simamia стоять за что-л. (кого-л.) mgawo (mi-) деление,

-fuzu добиваться успеха распределение

-kunjufu дружелюбный, -gombea 1) бороться

радушный, искренний за что-л., претендовать

jasiri смелый, отважный 2) быть кандидатом

jasiri (ma-) смельчак, храбрец -jiuzulu уходить в отставку

ujasiri (ед.) 1) смелость, храбрость; -tia sahihi подписывать

самоотверженность 2) риск mhariri (wa-) редактор

hiari (-) воля; волеизъявление insha (-) очерк

kwa hiari добровольно kura (-) 1) голосование

-jitolea 1) вызываться; жертвовать 2) голос (избирателя)

собой; посвящать себя чему-л. -piga kura голосовать

2) делать что-л. добровольно -apisha приводить к

-itika отзываться, откликаться присяге

-iga, -igiza подражать; -tapanya разбрасывать;

имитировать рассеивать

mchezo wa kuigiza пьеса; спектакль ufidhuli (ед.) надменность;

-sita 1) колебаться 2) внезапно дерзость

прекращать (начатое) usukani (ед.) руль

-ajiri нанимать на работу katibu (ma-) секретарь

ujira (ед.) жалованье, hila (-) хитрость, уловка

оплата труда -miliki владеть, обладать

-laumu обвинять; критиковать gavana (ma-) губернатор

mgomo (mi-) забастовка; -tisha, -tishia пугать;

саботаж угрожать

merikebu (-) корабль; судно; -dhibiti контролировать

пароход zama (-) время; эпоха

mchochezi (wa-) подстрекатель -zuka появляться, возникать

-chochea подстрекать; korti kuu верховный суд

провоцировать -churupuka ускользать;

-nyakua выхватывать, вырывать вырываться

makamo, makamu (мн.) возраст mgogoro (mi-) 1) конфликт

-tabiri предсказывать; предрекать 2) кризис

masafa (мн.) расстояние, hotuba (-) речь; выступление

дистанция -tema резать, рубить;

-susa, -susia бойкотировать колоть

uhamisho (ед.) 1) выселение, ссылка idara департамент; отдел

2) перевод (на другую работу) fursa (-) возможность; шанс

* * *

Урок 19. Somo la kumi na tisa


Грамматика

Служебные слова kunako, panapo, mnamo в функции предлогов.


Служебные слова kunako, panapo, mnamo, состоящие из субъектного приглагольного согласователя одного из локативных классов, недостаточного глагола -na и локативного форманта -po-, -ko-, -mo-, могут выполнять функцию самостоятельных предлогов, обозначающих временные понятия:

kunako mwaka huu “в этом году”;

panapo mwezi uliopita “в прошлом месяце”;

mnamo wiki hii “на этой неделе”;

mnamo saa kumi “в 4 часа”.

Следует иметь в виду, что слово mnamo имеет чисто временное значение, а слова kunako и panapo могут выполнять функции предлогов, имеющих пространственное значение, и в этом смысле они близки по значению к предлогам kwenye, katika и др. Например:

Napenda kupumzika kunako (kwenye) milima “Я люблю отдыхать в горах”;

Tulikutana panapo (katika) kituo cha basi “Мы встретились на автобусной остановке”.

Слово panapo имеет свою отрицательную форму – pasipo или pasina. В этом случае оно выступает в функции русского предлога “без”:

pasina sababu “без причины” (сравните: bila ya sababu);

pasipo maji “без воды” (сравните : bila ya maji).


Mazoezi

1. Дайте эквиваленты на суахили, употребив все возможные варианты перевода предлогов:

в этом году; в 5 часов вечера; в прошлом месяце; на озере; в другом городе; в конце века; у моря; на остановке; в утренние часы; в половине седьмого; без четверти 11; на вершине горы; без цели; без радости; без образования.


BIASHARA YA WATUMWA

Mwanzo wa kukutana kwa babu zetu na watu waliotoka nchi za ng’ambo unaonyesha kuwa ulikuwa katika karne ya kumi na tatu. Lakini inawezekana jambo hili lilitokea hata karne mbili au tatu kabla ya karne ya kumi na tatu. Sehemu ambayo wageni na wananchi walianza kukutana ilikuwa Kilwa ambayo inaonyesha* ilikuwa imekwisha twaliwa tangu karne ya kumi, labda hata mapema zaidi. Kilwa ulikuwa mji wa biashara iliyositawi. Vitu vilivyokuwa vinauzwa kwa kupelekwa nchi za ng’ambo vilikuwa pembe za ndovu, dhahabu na lulu. Biashara ya watumwa pia ilikuwa inaendeshwa Kilwa, hasa na Waarabu ambao walikuwa wamekwenda huko kwa madhumuni hayo. Watumwa walikuwa wanaletwa mwambao toka bara kama vile pembe za ndovu.

Waarabu walikuwa hawaendi bara mpaka karne ya kumi na tisa. Kwa hiyo pembe za ndovu na watumwa hao waliletwa mwambao na wananchi wa makabila fulani fulani, kutegemea nani kati ya makabila hayo alipigwa vita na wenzie na nani alimshika mwingine mateka. Pembe za ndovu na watumwa hao waliletwa mwambao. Waarabu walipewa vitu hivyo na watu hao kama zawadi. Waarabu waliwapa wananchi waliowaletea pembe za ndovu na watumwa zawadi za nguo, shanga, bunduki, waya za shaba, na kadhalika.

Basi utumwa ulikuwa umekwisha kuwa biashara ya maana ingawa biashara ya pembe za ndovu ilikuwa ni ya maana zaidi bado. Usakaji wa watumwa haukuanza mpaka labda sehemu ya mwisho ya karne ya kumi na nane wakati ambao koloni za Wafaransa zilipopata faida sana katika biashara hiyo. Baada ya hapo biashara ya watumwa ilianza kukolea sana katika sehemu za bara ya Kilwa. Waarabu walipata haja zao za watumwa toka kwa makabila yaliyoteka watu katika vita zilizokuwa zikipiganiwa baina ya makabila mbali mbali ya sehemu hizo. Kwa sababu hiyo vita baina ya makabila zilizidi kufuatana na mahitaji ya Waarabu juu ya watumwa.

Ni vigumu kusema kwa uhakika jinsi biashara hii ilivyokuwa inaendeshwa lakini yaonyesha* kwamba jinsi jambo lenyewe lilivyozidi kuwa ni la kawaida katika enzi hizo ndivyo utumwa ulivyoanza kuwa kama biashara ya kawaida. Matokeo ya biashara hii ya kishenzi yalikuwa mabaya sana na ya kusikitisha. Idadi ya wananchi wa sehemu za bara ya Kilwa ilipungua sana hata ikawa ni lazima, katikati ya karne ya kumi na tisa, wasakaji watumwa wasafiri siku kumi na nane hivi kabla ya kuvifikia vijiji walikoweza kupatikana watumwa.

Wananchi ndio waliokuwa wakitumiwa na Waarabu wachukue pembe za ndovu kuzipeleka hadi mwambao. Wachukuzi wa pembe hizo, kwa jumla, walikuwa wapagazi wa kuajiriwa. Lakini punde si punde idadi ya wapagazi ilipungua sana. Vijana wenye afya walikuwa wanatakiwa na makabila yao katika kazi ya ulinzi na kupigana vita na makabila mengine. Waarabu walihitaji sana wachukuzi wa pembe zao za ndovu na kwa sababu ya ukosefu ulioelezwa, Waarabu walianza kushika wananchi na kuwashurutisha wawachukulie pembe zao za ndovu. Wananchi wengi waliokamatwa hivyo waliteswa sana na wengi waliuawa au kufa katika misafara ya kwenda mwambao. Lakini inasemekana kuwa, kwa jumla, Waarabu walipata faida sana walipowauza hata hao watumwa wachache walioweza kufika mwambao.

Ni jambo la kushangaza kuwa Waarabu hao waliofanya biashara ya watumwa na pembe za ndovu hawakushughulika na mambo ya utawala. Lakini inafahamika kuwa wachuuzi wachache waliokata shauri kubaki nyuma na kuanza kuishi nchini walikuwa bado wanamtambua Sultani wa Unguja kama Sultani wao. Katika mwambao, Sultani alikuwa ameweka maafisa wake wa forodhani na kwa hiyo inajulikana kuwa yeye ndiye mtawala wa sehemu hizo.

Ni vigumu kusema kwa uhakika juu ya maafa yaliyoletwa na utumwa kwa wananchi kwa sababu mambo mengi ambayo tungesema yalitokana na uovu wa utumwa, yalikuwa ni matunda ya vita baina ya makabila mbali mbali pia. Vita maarufu ambazo zinajulikana kuwa zilileta maafa makubwa kwa wananchi ni kama zile za baina ya Wahehe na Wangoni huko kusini mwa nchi yetu. Mateka waliokamatwa na makabila mbali mbali katika vita kama hizo ndio waliofanywa watumwa wa kwanza wa Waarabu.

Pongezi kubwa ya kukomesha biashara ya watumwa ni budi** itolewe kwa Waingereza. Wao ndio walioanza kuishambulia biashara hiyo na wakapitisha sheria ya kuzuia biashara ya watumwa mwaka 1807. Toka hapo Waingereza walijaribu bila kupumua, na kwa moyo wote, kukomesha biashara hiyo ya aibu ingawa mara kwa mara katika jitihada zao ilikuwa lazima kufikiria hali ya uhusiano wao na mataifa mengine ambayo yalikuwa bado yanapendelea biashara hiyo iendelee. Lakini mwishoni mwa karne ya kumi na tisa juhudi zao zilianza kutoa matunda ya ushindi. Masoko yote ya watumwa yalifungwa na meli zilizokuwa zikichukua watumwa zilizuiwa zisipite katika njia fulani. Hata hivyo utumwa haukukomeshwa nchini mpaka Wadachi walipoanzisha serikali yao Tanganyika.


Maelezo

* Глагол -onyesha “показывать” в неопределенно-личной форме (inaonyesha; yaonyesha) может выполнять функцию вводного слова со значением “очевидно”, “видимо”, “судя по всему”.

** Существительное budi “избавление”, “выход” в современном языке суахили все чаще стало употребляться как синоним слова lazima “необходимость” для выражения модального значения, например:

Ni budi aende huko “Ему надо пойти туда”; (Ni) budi tuimalize kazi hii kwa haraka “Нам необходимо закончить эту работу быстро”.

Напомним, что слово budi передает значение долженствования в сочетании с отрицательной конструкцией глагола -wa na “иметь”: hana budi kwenda “он должен пойти”; hatukuwa na budi kumaliza “нам надо было закончить”.