Учебник соответствует разделу 2 (семестры 4-6) действующей обновленной Программы по языку суахили (основному) для студентов факультета международных отношений, уровень "Бакалавр"

Вид материалаУчебник
6. Переведите текст: Kibanga ampiga mkoloni
Kilwa kisiwani
Подобный материал:
1   ...   11   12   13   14   15   16   17   18   ...   26

Mazoezi

2. Переведите, используя выражения из текста:

судя по всему; город с процветающей торговлей; с этой целью; в зависимости от того, кто кого взял в плен; торговля бивнями все еще была на первом месте; захват рабов; они на этом сильно наживались; дела резко пошли в гору; в соответствии с потребностями; то, как велась торговля невольниками; в те времена; результаты оказались плачевными; постепенно; наемные носильщики; их заставляли работать; они подвергались тяжким мучениям; его признавали в качестве правителя; таможенные чиновники; страдания, причиненные народу; огромное зло; захваченные пленники; ему надо отдать должное; приняли закон о запрещении работорговли; позорный бизнес.


3. Замените предлог kwa направительной формой соответствующего глагола. Не забудьте поменять порядок слов там, где это необходимо:

1. Plau nzuri ya kuku iliyopikwa kwa mume. 2. Visa vilivyoelezwa kwa watoto. 3. Picha zinazochorwa kwa ajili ya rafiki. 4. Barua zilizoandikwa kwa mpenzi. 5. Nyimbo zitakazoimbwa kwa watalii. 6. Muziki uliopigwa kwa nyinyi. 7. Pesa zilizotengwa kwa jumuiya. 8. Teksti zinazotungwa kwa wanafunzi. 9. Vyombo vitakavyoletwa kwa mafundi. 10. Milango iliyofunguliwa kwa wageni.


4. Переведите, используя конструкцию с глаголом в направительной форме:

1. Праздник, устроенный в клубе для молодежи, был очень веселый. 2. Деньги, отправленные для новой партии, потерялись в дороге. 3. Товар, проданный вам на прошлой неделе, оказался нелегальным. 4. Песни, исполняемые для высокого гостя, рассказывают о национальных героях этой страны. 5. Еда, приготовленная для вас еще вчера, уже испортилась, так как было очень жарко. 6. Вещи, купленные для меня на рынке, отправьте в деревню моим родственникам.


5. Переведите следующие словосочетания, используя служебное слово -enye:

очень утомительный рассказ; интересные иллюстрации в книге; устрашающий голос; радостные мысли; вопрос, вызывающий удивление; закон, запрещающий политическую деятельность; цены, растущие вверх безостановочно; вечно почитаемые герои; страна, привлекающая массы туристов; грустная история; избираемые депутаты; быстро распространяющиеся новости; счастливый барабанщик; умный бухгалтер; самодостаточная нация; любимый десерт; счастливчик; удачливый бизнесмен; самоотверженные доноры.


6. Переведите текст:

Kibanga ampiga mkoloni

Zama za ukoloni palitokea mzungu mmoja. Mzungu huyo hakuwa mtu mwema. Alikuwa mkali na katili sana. Kwa ajili ya ukatili wake watu walimwita Mkoloni. Wananchi wote walimchukia sana popote pale alipokwenda.

Mzungu huyo alikuwa bwana shamba. Alikuwa na bakora ambayo kila alipokwenda kukagua mashamba, alikuwa na bakora hiyo mkononi. Alipendelea sana kuitwa ‘Bwana Mkubwa’. Mkoloni huyo alifurahia sana kupiga watu. Aliwapiga watu waliposhindwa kupalilia mashamba. Aliwapiga pamba yao ilipokuwa chafu. Aliwapa taabu sana.

Katika kijiji kimoja alikuwapo mzee mmoja aliyeitwa Kibanga. Mzee huyo alikuwa mwenye nguvu, hodari na shujaa. Alikuwa fundi wa mieleka. Ingawa alikuwa mwenye nguvu, alikuwa mpole. Hivyo watu wa kijiji hicho walimpenda na kumtegemea kuwaongoza vitani.

Siku moja yule mzungu alifika kijijini kukagua mashamba ya mihogo. Jumbe pamoja naye wakatembelea mashamba. Kwa bahati mbaya mwaka ule haukuwa na mvua ya kutosha. Kwa hiyo mihogo haikusitawi. Kila wakati yule mzungu alipotazama mashamba alitikisa kichwa na kufoka. Mwisho akamwagiza jumbe kuitisha mkutano wa watu wote wa kijiji. Waliporudi kijijini jumbe akapiga mbiu. Watu wote wakakusanyika. Walipofika tu, yule Mkoloni akaanza kuwatukana, akawaambia, ‘Nyinyi watu weusi ni wavivu sana. Hamfanyi kazi sawa sawa. Mashamba yenu ni mabaya sana.’ Jumbe akataka kumjibu ili kumweleza kwa nini mihogo haikusitawi. Kabla hajamweleza yule mzungu alimrukia na kumpiga kofi. Kisha akasema, ‘Sitaki kujibiwa na wewe, mvivu wa wavivu.’ Watu wote wakakaa kimya. Hakuna aliyeweza kufanya kitu.

Kibanga akajitokeza, akasimama. Akamtazama yule Mkoloni kwa dharau sana. Kisha akamwuliza, ‘Kutuita sisi wavivu ndiyo nini? Na kumpiga umbe wetu mbele yetu, maana yake nini?’

Kabla ya kumaliza kusema, Mkoloni aliamka kitini kwa hasira, akataka kumpiga Kibanga. Alishika bakora yake mkononi. Akasema, ‘Nitakuadhibu vibaya kima we! Unajifanya kuwa shujaa? Huwezi kucheza na bwana mkubwa. Nitakupiga, kisha utakwenda jela miezi sita.’ Lakini Mkoloni hakuwahi kumwadhibu Kibanga. Aliadhibiwa yeye. Kabla ya kumfikia, Kibanga alimpiga chenga. Kisha akamrukia, akamnyang’anya bakora yake. Akaitupa, ikaokotwa na vijana, wakaificha.

Kibanga alimshika yule mzungu akamwambia, ‘Wewe umezoea kutoa amri kila siku, lakini leo utashika adabu, mbwa wee!’ Papo hapo alimnyanyua juu na kumbwaga chini, puu! Yule Mkoloni akaumia sana. Kabla ya kuamka, Kibanga alimwinua tena na kumbwaga chini kama furushi la pamba. Akamkalia.

Hapo yule Mkoloni akawa hana la kufanya. Bila ya bakora alikuwa hana nguvu. Akaomba radhi akilia, ‘Samahani! Naumia! Nihurumie! Sitafanya tena hivyo.’ Kibanga alimjibu kwa dharau, ‘Sikuachi mbwa wee! Leo utaona cha mtema kuni! Ulijiona una nguvu. Leo nitakutengeneza.’

Wazee wakamshika Kibanga na kumwomba asimpige tena. Akamwacha. Kwa shida yule Mkoloni alijivuta kwenda hemani. Alikuwa amejaa vumbi huku damu zikimtoka. Wazee wengine wakamfuata nyuma. Walinyamaza kimya, wakimhurumia. Lakini vijana walifurahi sana. Baadaye waliimba wimbo wa kumsifu Kibanga.

Jioni yule Mkoloni aliomba radhi kwa wazee. Mzee mmoja akasimama na kumwambia, ‘Umefanya vizuri kuomba radhi, nasi tunaipokea. Lakini tangu leo usijivunie ubwana. Jivunie utu. Nyinyi wakoloni mna kiburi. Mnatudharau. Kama ungetuuliza tungekuambia kwa nini mihogo haikusitawi. Haya yote yamekupata kwa sababu ya kiburi chako.

Baada ya hapo wazee wakamsamehe, lakini hawakumpa bakora yake. Ikabaki nyumbani kwa Jumbe.


7. Дайте русские эквиваленты:

-chukia mtu; mtu mkali na katili; -kagua mashamba ya mihogo; -palilia mashamba; -mpa mtu taabu; fundi wa mieleka; -wa mpole; -tikisa kichwa na kufoka; -agiza kuitisha mkutano; -piga mbiu; -piga mtu kofi; -tukana sana; -tazama kwa dharau; -jitokeza; -sema kwa hasira; -adhibu vibaya; -mpiga chenga adui; -nyanyua mzigo; -nyanyua mkono; -bwaga chini; -omba radhi; -ona cha mtema kuni; -mhurumia mtu; -jivunia ubwana; -jivunia utu; -ona kiburi; mtesa mtu mpaka afe; -shurutisha kwa nguvu; mgogoro umekolea; sheria za kishenzi; -sababisha maovu.


8. Перескажите в лицах историю из текста “Kibanga ampiga mkoloni”.


9. Переведите:
  1. Судя по всему, еще в 13-ом веке предки современных танзанийцев начали продавать заезжим торговцам бивни слонов, золото и жемчуг для отправки в заморские страны.
  2. Местное население поставляло арабам невольников и взамен получало от них подарки в виде тканей, бус, ружей, медных проводов и другой утвари.
  3. Результаты работорговли, которая велась варварским образом, были очень плачевными, поскольку население района Килвы очень сократилось.
  4. Охота за рабами достигла наивысшего расцвета в конце 18-го века, как раз в то время, когда работорговля стала очень выгодной для французских колонизаторов.
  5. Арабы испытывали острую нужду в носильщиках, поэтому они хватали крепких мужчин из числа местного населения и заставляли их работать на себя.
  6. Пленники, которых забирало племя, победившее в междоусобной войне, становились первыми, кого продавали арабам как товар.


Msamiati

lulu (-) жемчуг; жемчужина -nyanyua поднимать

waya (-; nyaya) провод; кабель uovu (ma-) вред; зло

mwambao берег (морской), mpagazi (wa-) носильщик

побережье (груза на голове, плечах)

-kolea накаляться (прям. и перен.) forodha (-) таможня

mshenzi (wa-) дикарь, варвар mieleka, miereka (-) борьба

-a kishenzi дикий, варварский (спортивная)

-shurutisha заставлять, -adhibu наказывать

принуждать mbiu (-) сигнальный рог

-tesa мучить, причинять боль -piga mbiu оповещать

teso (ma-) страдание, боль; пытка -piga chenga ускользать;

maafa (мн.) беда, несчастье; уклоняться

катастрофа kiburi (vi-) высокомерие,

-ona cha mtema kuni узнать, надменность

почем фунт лиха (идиома) pongezi (-) 1) поздравление

-omba radhi просить 2) приветствие

прощения -tukana 1) ругать,

-foka 1) бить ключом, оскорблять 2) ругаться,

пениться 2) извергаться браниться

3) кипеть негодованием -bwaga сбрасывать,

-piga kofi (ma-) давать пощечину сваливать (вниз, на землю)

-jitokeza 1) показываться, -saka гнаться, преследовать;

появляться 2) выходить вперед вылавливать

* * *

Урок 20. Somo la ishirini

(marudio)


1. Переведите текст:

KILWA KISIWANI

Kilwa Kisiwani ni moja ya miji mingi ya zamani ambayo ni kivutio cha watalii na watafiti wa mambo ya kale. Kilwa Kisiwani imeendelea kubeba majengo ya zamani yakiwa na historia ya zaidi ya miaka 9,000 iliyopita.

Kwa sasa, majengo hayo ni magofu, yakiwa yamebaki kuwa sehemu ya watalii na watafiti kujionea jinsi jamii za watu wa zamani zilivyoishi, sambamba na zilivyokuwa zikiendesha maisha ya kila siku.

Kilwa Kisiwani ilianza kupata umaarufu wake katika karne ya tisa, baada ya kununuliwa na mfanyabiashara Ali bin Al-Hassan kutoka kwa wazee wa jadi waliokuwa wakiimiliki.

Mara baada ya kununua Kilwa Kisiwani, mfanyabiashara huyo kutoka mashariki ya mbali, alijenga himaya kubwa ya kiuchumi katika ukanda wa pwani ya Afrika ya Mashariki na miji ya kando kando ya bahari ya Hindi.

Biashara kubwa ambazo ziliendeshwa na himaya hiyo zilikuwa zile za utumwa, pembe za ndovu, nguo, tende, dhahabu na shaba, vitu ambavyo viliuzwa katika masoko ya uarabuni.

Katika karne ya 13 chini ya utawala wa familia ya Mahdali Kilwa Kisiwani ilikuwa maarufu na umaarufu wake uliifanya ifahamike katika nchi nyingi za kusini na kaskazini mwa bara la Afrika.

Umaarufu wa Kilwa Kisiwani ulimfanya mtafiti Abu Abdullah Ibn Battuta kuitembelea mwanzoni mwa mwaka 1330, ambapo aliamua kuwekeza katika shughuli mbalimbali za biashara ikiwa ni pamoja na kushawishi wafanyabiashara kutoka nje kuja kuitembelea ili wawekeze pia.

Utawala wa Kiarabu katika kisiwa hicho ulikoma kwa muda katika karne ya 14 baada ya Vasco da Gama kufika kama mtafiti na baadaye kuwashawishi Wareno wenzake kuvamia ili wawekeze. Mkakati huo ulipofanikiwa, Kilwa ilijikuta mikononi mwa Wazungu kwa mara ya kwanza.

Wareno walikitawala na kufanikiwa kuhamisha kiasi kikubwa cha madini na vitu vya asili kama shanga na mavazi vilivyokuwa vikiuzwa kwa ajili ya matumizi ya miji iliyochipukia kusini mwa Afrika.

Hata hivyo, utawala wao haukudumu sana, kwani mwanzoni mwa mwaka 1512 Waarabu wakiwa na jeshi kubwa walikivamia tena na kukichukua.

Wakati wa utawala wao, Waarabu waliurejeshea hadhi iliyokuwa imepotea. Mwaka 1784, mtawala wa Oman alikichukua kisiwa hicho na kile cha Zanzibar kwa nia ya kutanua biashara zake, ambapo aliweka utaratibu mpya wa kulipa kodi na ushuru kwa watu na wafanyabiashara waliokuwa wakiingia na kutoka.

Katika juhudi za kujiimarisha, aliwatumia Wafaransa kumjengea kituo cha kijeshi na ngome kubwa aliyoifanya kuwa mahali pa kujificha na kuhifadhi dhana za kijeshi.

Historia ya kisiwa hicho inaonyesha kuwa, kati ya mwaka 1881 hadi 1918 kilikuwa chini ya uangalizi wa Ujerumani, sambamba na maeneo mengine ya Tanzania bara ambapo Zanzibar ilibaki mikononi mwa Sultan wa Oman aliyekuwa na makazi yake Unguja.

Hadhi ya Kilwa Kisiwani ilipotea ghafla mara baada ya Wajerumani kuondoka. Inaelezwa kwamba kutokana na historia mbaya ya mauaji iliyoendeshwa na watu hao, haikuwaumiza vichwa Waingereza kukiendeleza kisiwa hicho.

Badala yake, waliweka silaha nzito katika pwani ya Kilwa na kuzielekeza kisiwani hapo ili kuwaogopesha wavamizi. Majengo na vitu vilivyoko huko viliendelea kuharibika kadiri siku zilivyokwenda.


2. Найдите в тексте эквиваленты следующих выражений:

достопримечательность, представляющая интерес для туристов и изыскателей древностей; от построек остались руины; ознакомиться с образом жизни других людей; старейшины; в чьих руках он (город) находился; подконтрольная экономическая зона; прибрежная полоса Восточной Африки; вкладывать деньги в торговую деятельность; арабское господство закончилось на какое-то время; когда эта тактика удалась; города, возникавшие на юге Африки; их власть продержалась недолго; арабы вернули свои позиции; шире развернуть торговую деятельность; новый порядок уплаты налогов и пошлин; построить военизированную крепость; оберегать военные секреты; находиться под контролем Германии; одновременно с другими территориями; для острастки захватчиков; день ото дня.


3. Дайте русские эквиваленты:

-tafiti mambo ya kale; mtafiti wa lugha za nadra; -geuka magofu; gofu la mtu; -jionea kwa macho yako mwenyewe; himaya ya kiuchumi; -enda sambamba; -endelea sambamba; -funga ukanda; ukanda wa pwani; kanda za kaskazini; -wekeza katika maendeleo ya sayansi; shughuli zimekoma; -komesha utawala wa kikatili; -vumbua mkakati mpya; mkakati wa kuendesha vita; kuchipuka kwa miji mipya; majira ya machipuko; -tanua eneo la miliki; -tanua kinywa; -kumbana na upinzani mkali; -kumbana na shida za maisha; chama cha upinzani.


4. Переведите вопросы и дайте на них ответы на суахили:

1. Каков примерно возраст города Килва? 2. Что сейчас представляет собой этот город? 3. Благодаря чему Килва Кисивани получил свою первоначальную известность? Когда это было? 4. Какая экономическая деятельность велась вдоль побережья Восточной Африки во времена, когда она находилась под контролем торговцев с арабского востока? 5. Как развивалась история Килва Кисивани в 13-14 веках? 6. Каким образом этот город оказался в руках европейцев? 7. Как долго португальцы хозяйничали на острове Килва? 8. Какие порядки установил правитель Омана на островах Килва и Занзибар и с какой целью? Когда это было? 9. Кто ему помогал в попытках закрепить свое господство? 10. Под чьим контролем оказалась континентальная часть Танзании в конце 19 начале 20 веков? 11. Что происходило на Занзибаре в это время? 12. Каков был вклад англичан в развитие острова Килва?


5. Переведите следующий текст письменно:

Kuhusu asili ya utamaduni wa Pemba

Vijiji ambavyo vinafaa vijadiliwe kwa undani zaidi na watafiti wa historia ya Pemba, ni Kiuyu na Micheweni. Sababu kuu iliyojitokeza ni kuwa vijiji hivyo vinakaribiana sana. Pamoja na hayo Kiuyu kinaelekea kuwa ndicho kijiji au ndio lango lililowapokea wageni wa mwanzo na kuwakaribisha ndani ya kisiwa cha Pemba.

Uchunguzi uliofanywa na watafiti katika Kiuyu na Micheweni ulionyesha kuwa vijiji hivi viwili vina utamaduni mchanganyiko. Upo utamaduni ambao unaweza kufananishwa na ule unaoweza kupatikana Tanzania bara na pia upo utamaduni wa Kiarabu. Dini ya Kiislamu ndiyo dini inayotawala. Watu wa maeneo hayo ya Pemba hawakuchanganyika sana damu na kisura na kiumbile, wanaelekea kuwa Wabantu zaidi kuliko Waarabu. Hata hivyo, tabia zao, mavazi na desturi zao nyingi zimeelekea katika utamaduni wa Kiarabu. Ngoma na nyimbo zao zimekuwa katika hali ya mchanganyiko wa Ubantu na Uarabu.

Kwa jumla, upo ushahidi wa kuonekana kwa macho, kama watu, vitu nakadhalika, ambao unadhihirisha kuwa maeneo hayo yana uhusiano wa muda mrefu sana na Uarabuni. Kutokana na ushahidi wa kihistoria uhusiano au aina hiyo ya utamaduni mseto ulikuwepo kwa muda mrefu. Taarifa hizo za kihistoria zilizoandikwa zinaonyesha kuwa baina ya miaka 700-850 tayari utamaduni wa Waswahili ulikuwepo na ulikuwa umekwishaathiriwa na Waarabu.

Ushahidi mwingine unaeleza kwamba yalikuwepo maingiliano ya kibiashara na ya ndoa baina ya watu wa asili mbalimbali waliokuwa wakiishi pwani. Miongoni mwa Waswahili wenyewe inawezekana kuwakuta watu wenye asili ya Kishirazi itokayo Uajemi.

Jambo ambalo bado linabakia kuwa na utata kwenye utafiti ni kwamba hakuna maelezo thabiti kuhusu watu hao walivyoishi pamoja na ni nani aliishi hapo kwanza.

Kutokana na taarifa za mapokeo kutoka kwa wazee wa Micheweni, wanavyofahamu wao, ni kuwa wakati walipofika watu kutoka Mrima, watu ambao walidai kuwa ni Washirazi, Pemba ilikuwa haina watu. Taarifa za wazee hao zinadai kuwa Washirazi ndio watu wa kwanza kufika Pemba.

Lakini kufuatana na taarifa za historia zilizoandikwa, kabla ya kuja Washirazi mnamo mwaka 1100 tayari misikiti ya mwanzo ya mawe ilikuwa imekwishajengwa na kuwa Pembe ilikuwa ni mojawapo ya makao ya mwanzo ya Kiislamu Afrika ya Mashariki.Washirazi walifika Pemba kwa kutumia jahazi wakitokea Uajemi.


6. Подберите синонимы к подчеркнутым словам:

-karibiana sana; sababu iliyojitokeza; utamaduni mchanganyiko; dini inayotawala; -changanyika damu, kisura na kiumbile; ushahidi unaodhihirisha; maingiliano ya kibiashara; jambo lenye utata; -fanya utafiti.


7. Переведите:
  • Танганьика получила свою независимость 9 декабря 1961 года почти после векового господства германских и английских колонизаторов. Это стало результатом сложной, длительной и самоотверженной борьбы народа, желавшего добиться свободы и права на уважение.
  • В историю борьбы за независимость вошло имя героя Мквава, который на протяжении десяти лет конца 19 века мужественно противостоял германским колонизаторам вместе со своими соплеменниками. Но, поскольку силы были неравные, Мквава потерпел поражение и предпочел смерть унижению от врага.
  • Еще одну героическую страницу в историю антиколониальной борьбы в Восточной Африке вписали участники восстания Маджи Маджи (vita vya Maji Maji) в период 1905-1907 годов. В этом движении как никогда ранее проявился дух единения народа Танганьики. Около 20 народностей южных районов страны, объединившись, выступили против германских колонизаторов. К сожалению, им не хватило четкого руководства и хорошей организации, и восстание было жестоко подавлено.
  • После второй мировой войны народу Танганьики пришлось добиваться своего права на независимость у англичан, которые правили в этой стране с 1917 года. Политическая партия ТАНУ под руководством Дж. К. Ньерере довела эту борьбу до победного конца.
  • Ньерере, умерший в 1999 году, был не только выдающимся лидером своего народа, но и мудрым политиком, признанным во всем мире за его огромный вклад в дело прогресса и независимости в Африке.


8. Переведите и озаглавьте следующий текст. Перескажите его на суахили:

Baada ya waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika Julius Kambarage Nyerere kujiuzulu wadhifa huo, kazi kubwa aliyoifanya ni kuzunguka nchi nzima. Katika kazi hiyo hakuacha kijiji kikubwa wala kidogo, alifika kila pembe ya Tanganyika ambako alikuwa na jukumu kubwa la kuwaelemisha wananchi faida na jinsi ya kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Alikuwa akitoa elimu kubwa juu ya kujitegemea ikiwa Watanganyika wanataka maendeleo ya haraka. Aliwaeleza wananchi, katika kila kijiji alichotembelea kwamba maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe.

Mwalimu Nyerere alisema kuwa baada ya uhuru kupatikana, Tanganyika haikuwa tena na wajomba wala shangazi ambao wangeweza kuleta maendeleo.

Alieleza kuwa wakati wakoloni wakitawala kwa ufidhuli ardhi ya Tanganyika na watu wake, waliweza kuleta maendeleo kidogo, hasa sehemu ambazo waliona wana maslahi makubwa kwa ajili ya maendeleo ya nchi zao.

Ni kutokana na sababu hizo, maendeleo katika eneo moja hadi jingine yalikuwa yakitofautiana mno kufuatana na umuhimu wake kwa wakoloni. Katika mazingira hayo, maeneo ambayo yalikuwa yakitumika kwa uzalishaji wa mali kwa wakoloni yalikuwa na huduma za jamii kuliko maeneo mengine.

Maeneo yaliyokuwa yakiwazalishia mali wakoloni yalikuwa na barabara nzuri, hospitali nzuri kwa ajili yao na nyingine za hali ya chini kwa ajili ya wafanyakazi wao wanapougua. Baadhi ya maeneo ya namna hiyo pia yalikuwa na umeme, maji na nyumba nzuri walizokuwa wakiishi.

Katika maeneo ya vijijini aliyotembelea, Mwalimu Nyerere alitumia kila aina ya usafiri uliokuwepo na uliowezekana kulingana na mazingira kwa wakati huo. Alipanda punda, aliendeshwa katika baisikeli na pia alitembea kwa muda mrefu hadi anamaliza mizunguko hiyo ambayo inaelezwa ilimchukua zaidi ya miezi mitano.

Kila kijiji alichokuwa akipita, Mwalimu Nyerere alishirikiana na wenyeji katika kilimo, aliwaonyesha na kuwaelekeza namna kilimo bora kinavyoweza kuwaongezea mapato na pia alishiriki katika ujenzi wa barabara na majosho.

Kiongozi huyo wa TANU katika kuonyesha mfano, alishika jembe, alipanda mbegu, alivuna na alishiriki katika kuanza ujenzi wa majengo ya shule ama zahanati.

Katika kazi hiyo ya kuzunguka nchi nzima, Nyerere pia alijaribu kutoa ushawishi kwa wanavijiji kuishi jirani jirani ili serikali iweze kutoa huduma zinazowezekana kwa urahisi zaidi. Hili baadaye lilikuja kuwezekana na kuonyesha mafanikio makubwa.


9. Закончите следующие предложения, выбрав подходящий вариант из скобок:
  1. Utawala wa kikoloni ulianzishwa pwani ya Afrika ya Mashariki na (Waarabu; Waingereza; Wareno).
  2. Wazungu wa kwanza walifika Afrika ya Mashariki ili kuyashuhudia kwa macho mambo yake ya ajabu (karne 4 hivi nyuma; kati kati ya karne ya 19; mwanzoni mwa karne ya 20).
  3. Watu wa misheni walikuja Afrika kwa madhumuni ya (kufanya uchunguzi wa bara hili; kueneza dini ya Ukristo; kufanya biashara ya watumwa ipigwe marufuku).
  4. Mzungu aliyependwa na kuheshimiwa kuliko wote na wenyeji ni (Richard Burton; Speke; David Livingstone; Stanley).
  5. Mwaka 1890 sehemu ya pwani ya Afrika ya Mashariki ilinunuliwa na Wadachi kutoka kwa (mtawala wa Unguja; Waarabu wa Oman; wakoloni wa Uingereza).
  6. Waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru alikuwa (Julius Nyerere; Rashidi Kawawa; Sheikh Abeid Amani Karume).
  7. Shujaa maarufu wa Afrika aliyejulikana kwa jina la Mkwawa (alinyongwa na wanajeshi wa Kijerumani; alifungwa jela kisha akatoroka; alijiua mwenyewe asije akakamatwa).
  8. J. Nyerere aliiacha kazi ya ualimu kwa sababu alitaka (kuwa mfanya biashara; kujizamisha katika mambo ya siasa; kufanya kazi ya uhariri gazetini).
  9. Sheikh Amani Abeid Karume amepata umaarufu kati ya wananchi wote wa Unguja kwa vile (alivyokuwa baharia jasiri; alivyofundisha watu elimu mbali mbali; alivyoanzisha ushirika halisi wa wafanya kazi).
  10. Pongezi nyingi za kukomesha uovu wa biashara ya watumwa ziwaendee (Waingereza; Waarabu; Wadachi) ambao walipitisha sheria ya kuzuia biashara hiyo mnamo mwaka (1910; 1860; 1807).
  11. Watu wa kwanza wanaodhaniwa kuingia kisiwani Pemba walikuwa (Waarabu; Washirazi, Wahindi).
  12. Dini inayotawala kisiwani Pemba ni (Uislamu; Ukristo).