Учебник соответствует разделу 2 (семестры 4-6) действующей обновленной Программы по языку суахили (основному) для студентов факультета международных отношений, уровень "Бакалавр"

Вид материалаУчебник
Vi. utibabu, elimu na mambo ya dini
Mwafrika mmoja “У него появилось много друзей, среди них
Usitawi wa mambo ya utibabu
Kuwapo kwake mkutanoni kuliwashangaza watu wengi “Его присутствие на собрании удивило многих”; Waziri alisisitiza kuwako
5. Переведите и перескажите следующие тексты: Hospitali ya Ocean Road
Chanjo ya homa ya manjano haina haja tena
Подобный материал:
1   ...   12   13   14   15   16   17   18   19   ...   26

10. Переведите:
  1. Багамойо, бывшая столица Восточной Африки немецкого периода, находится в 75 км к северу от Дар эс Салама, на противоположном Занзибару берегу.
  2. Когда-то город Багамойо был известным центром работорговли благодаря своей хорошей природной гавани, идеальной для судоходства и мореплавания.
  3. Первым каменным зданием в Багамойо была старая тюрьма у берега океана, где под землей толпы рабов ожидали прихода арабских судов.
  4. Город Багамойо также был отправным пунктом для первых европейских исследователей на их пути к поискам истоков Нила. Такие известные исследоватили Африки, как Ливингстон, Стэнли, Бартон, Спик побывали в Багамойо.
  5. Туристов привлекает музей с замечательной коллекцией фотографий и сувениров, относящихся к Ливингстону и немецкому колониальному периоду.
  6. Башня первой католической церкви в Восточной Африке также расположена в Багамойо. Это башня носит имя Ливингстона, поскольку здесь одну ночь находилось его тело перед отправкой в Лондон.
  7. Одной из достопримечательностей Багамойо являются руины Каоле, которые состоят из развалин двух мечетей и около 30 могил.
  8. Таможня и склад также были построены немцами в конце 19 века. На развалинах склада сохранились чаши, которые когда-то были заполнены керосином для того, чтобы крысы не проникали в складские помещения.


11. Познакомьтесь с суахилийскими пословицами и переведите их. Обратите внимание на модель словообразования существительных:
  • Mchezea moto humteketeza
  • Mtaka yote hukosa yote
  • Mchimba kisima hakosi maji
  • Mchomwa mwiba haendi tena
  • Mchunga farasi usipande punda
  • Mpanda ngazi hushuka
  • Msema kweli hakosi
  • Mzoea punda hapandi farasi


12. Подготовьте сообщения на темы:

А/ Исторические этапы развития Танзании;

B/ Выдающиеся лидеры Танзании;

С/ Исторические места Восточной Африки.


Msamiati

-tafiti изучать, исследовать -kumbana na сталкиваться,

mtafiti (wa-) исследователь, наталкиваться

изыскатель upinzani (ед.) 1) оппозиция,

gofu (ma-) развалины, руины противодействие

-jionea увидеть воочию; 2) протест, сопротивление

убеждаться в чем-л. tende (-) финик

silaha (-) 1) оружие 2) орудие -wekeza инвестировать,

sambamba 1) параллельно вкладывать деньги

2) одновременно, вместе mseto (mi-) смесь,

ukanda (kanda) пояс, район, зона смешение

maingiliano (мн.) 1) связи, Ushirazi (ед.) г. Шираз

взаимоотношения Mshirazi (wa-) потомок

2) взаимопроникновение перса из Шираза

-tanua расширять, раздвигать utata (ед.) 1) неясность,

-chipuka 1) распускаться, неопределенность

прорастать (о растениях) 2) путаница, сложность

2) появляться, возникать (перен.) mapokeo (мн.) предание,

dhana (-) 1) мысль, идея; устное народное творчество

точка зрения 2) концепция mkakati (mi-) тактика

-nyanyasa глумиться, wadhifa (nyadhifa) пост,

издеваться, унижать должность

unyanyasaji (ед.) угнетение, josho (ma-) место для

притеснение умывания, стирки, мытья

* * *

VI. UTIBABU, ELIMU NA MAMBO YA DINI

Здравоохранение, образование, религия


Урок 21. Somo la ishirini na moja

Грамматика
  1. Аналитические глагольные конструкции с показателем -ki- во вспомогательном глаголе -wa.
  2. Глагол -wa в глагольных конструкциях, передающих значение “в том числе, включая” и т.п.


Вспомогательный глагол -wa в аналитических конструкциях, оформляясь показателем условного наклонения -ki-, указывает на одновременность протекания действия, выраженного смысловым глаголом придаточного предложения, с другим действием, передаваемым глаголом главного предложения. При этом смысловой глагол придаточного предложения может быть оформлен показателем -na- (многократность, регулярность действия на момент речи) или -me- (завершенность действия к моменту речи или состояние в тот момент). На русский язык такие сложные глагольные конструкции можно переводить причастиями или деепричастным оборотом. Например:

Utaweza kuona magari mengi barabarani yakiwa yanachukua abiria “Ты сможешь увидеть на улице много машин, перевозящих пассажиров”;

Yakiwa yamepandwa kwa wakati wa kufaa, maua haya hayatakosa kusitawi majira yote “Посаженные вовремя, эти цветы непременно будут цвести весь сезон”;

Akiwa amejawa na hofu Tegu alijibu “Почувствовав страх, Тегу ответил”.

Отрицание в таких конструкциях осуществляется во втором компоненте, т. е. смысловом глаголе:

Tegu, akiwa bado hawezi kusema kwa kuduwaa alimfuata baba yake “Будучи все еще не в состоянии говорить от удивления, Тегу последовал за своим отцом”.


В суахили существует несколько глагольных форм, с помощью которых можно выразить такие значения как “в том числе, в их числе, включая, среди них” и т.п. Например, конструкция глагола -wa в сочетании с показателем условного наклонения -ki- и конечным локативным релятивом -po/-mo – -kiwapo/-kiwamo (и их фонетические варианты -kiwepo/-kiwemo), где согласование осуществляется по класу существительного, о котором идет речь, и которое следует за этой глагольной формой. Например:

Safarini nimenunua vitu kadhaa ikiwamo ramani ya Kenya “Во время путешествия я купил несколько вещей, в том числе карту Кении”;

Amepata rafiki wengi akiwapo Mwafrika mmoja “У него появилось много друзей, среди них один африканец”.

В другой конструкци с тем же значением, ikiwa ni pamoja na, глагол -wa, как правило, стоит в неопределенно-личной форме. Но могут встречаться и личные формы, где согласование осуществляется по классу существительного, которое занимает препозицию по отношению к этому союзному слову. Сравните:

Amepata rafiki wengi ikiwa ni pamoja (wakiwa ni pamoja) na Mwafrika.

Надо заметить, что в обеих этих конструкциях согласование возможно по одному из локативных классов, обычно ku- или mu-. Приведем для сравнения предложение – “В его столе много разнообразных предметов, в том числе и острый нож”, которое имеет несколько возможных вариантов перевода:

Mezani mwake mna vitu mbali mbali kikiwemo (mkiwemo) kisu kikali; …vikiwa ni pamoja na kisu kikali; … ikiwa ni pamoja na kisu kikali; … kukiwa ni pamoja na kisu kikali.


Mazoezi

1. Переведите:

1. Nilipofika kwa mjomba wangu wakati wa likizo nilimkuta akiwa anashughulika na ujenzi wa boma la maji. 2. Katika bandari tuliwaona wapagazi chungu nzima wakiwa wanabeba mizigo na vitu vingine. 3. Walipokuwa wakiishi pwani ya bahari walizoea kuona meli za kigeni zikiwa zinapakua na kupakia bidhaa mbali mbali. 4. Nikiwa nimejaa furaha tele kwa ajili ya zawadi niliyonunuliwa nikamkimbilia mamangu na kumbusu. 5. Ukiwa umepotea njia uwaulize wenyeji au usipowakuta, tumia simu ya mkono niliyokupa ukaniulize mimi. 6. Alifanya hatua nyingine kadhaa akasimama akiwa hajui la kufanya kwa jinsi alivyoshtuka kumwona joka mkubwa ajabu akiwa anamsogelea pole pole. 7. Usimsumbue kaka yako kwa maswali ya kipumbavu akiwa anajiandaa kwa kupasi mitihani ya chuo kikuu. 8. Afadhali wajifunze namna ya kutumia kompyuta wakiwa wanajifunza bado na wenye uwezo wa kufahamu mambo upesi upesi. 9. Tutashindwa kuukamilisha ujenzi wa daraja hili tukiwa tumeishiwa na pesa zote.


2. Переведите предложения, используя формы -kiwamo/ -kiwapo или -kiwa ni pamoja na:

1. Каждое утро я читаю все газеты, которые мне приносят домой, включая и газету “Ухуру”. 2. Рабочие, объявившие забастовку, требовали предоставить им больше прав, в том числе право на бесплатное лечение. 3. В своем выступлении главный врач подчеркнул некоторые актуальные вопросы, в том числе и проблему отсутствия средств на строительство родильного дома. 4. Принимая присягу, новый президент обещал сделать важные шаги, включая меры по предотвращению экономического кризиса. 5. В этой маленькой стране есть много полезных ископаемых, включая медь и золото. 6. Он объявил о своей добровольной отставке, называя много причин, среди них несогласие с политикой, проводимой правящей партией.


USITAWI WA MAMBO YA UTIBABU

Uganga ni kitu ambacho watu wa kila sehemu ulimwenguni walikuwa nacho tangu awali. Babu zetu walishambuliwa na magonjwa pia. Toka hapo kale babu zetu walitumia dawa za miti shamba kuponya maradhi au kupunguza maumivu. Kwa vile maisha yao yalikuwa ya taabu taabu iliwabidi wajue dawa nyingi. Walijua dawa za kuponya mtu akiumwa na nyoka, tandu au nge. Walijua dawa za kuponyesha maumivu ya tumbo au kichwa. Inasemekana pia kuwa walijua dawa za magonjwa kama kichaa au kurukwa akili.

Hapo kale uganga ulikuwa ni kazi iliyorithiwa. Mtoto mkubwa wa mganga alirithi uganga wa baba yake na akiwa yungali hai*, baba huyo aliambatana sana na mtoto wake mkubwa, mara nyingi wa kiume, ili amwonyeshe jinsi sayansi ya kuponya maradhi ilivyokuwa inaendeshwa na miti shamba ambayo ilitumiwa kuponya maradhi mbali mbali. Bila ya shaka wataalamu wa siku hizi wangelipenda kudadisi kama kweli miti shamba hiyo ilikuwa ni dawa ya maradhi fulani.

Jitihada kubwa ilifanywa na serikali ya Wadachi kuanzisha na kusitawisha mambo ya utibabu wa kisasa nchini. Idara ya utibabu ilianzishwa kwa mara ya kwanza na Wadachi tarehe 1 Aprili, 1891 wakiwapo madaktari watano na watumishi wa hospitali kumi na wanne wa Kidachi. Hospitali ndogo ndogo kadha wa kadha zilianzishwa katika sehemu kubwa ya Tanganyika. Kusudi kubwa la Idara hiyo wakati huo lilikuwa kutibu watumishi wa serikali, lakini pia ilitambulikana kwamba mipango ya kuweka kinga kwa magonjwa ni ya muhimu sana katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Kazi iliyoikabili Idara ya utibabu ilikuwa kubwa sana lakini ukosefu wa fedha ulizuia upanuaji wa kazi hizo. Hali ya usafi na kanuni za afya zilikuwa mbaya sana hasa katika miji mikubwa ya Tanga na Dar es Salaam. Lakini kwa ajili ya ukosefu wa fedha, mifereji ya maji na kazi za kuondoa uchafu na kuua mbu hazikuweza kuongezwa.

Vita kuu ya pili pia ilizuia maendeleo ya Idara ya utibabu. Madaktari kumi na mmoja walichukuliwa vitani na kazi zote za dawa zilipunguzwa. Lakini wagonjwa walizidi sana kwenda hospitali kupata matibabu. Ingawa hivyo yalikuwapo mafanikio mema fulani. Kazi iliyokuwa ya maana sana ilikuwa ni kutiliwa mkazo kwa ubora wa chakula kizuri kwa mwili na magonjwa yanayotokana na kutokula chakula cha kutosha na cha kufaa.

Baada ya vita, Idara ya utibabu ilifanya maendeleo mazuri ingawa mambo mengine mabaya, kwa mfano kuwa na hospitali mbali kwa Wazungu, yalikuwa bado yapo. Kazi za dawa hazikutosheleza mahitaji ya watu kwa vile ambavyo watu wengi walikwenda hospitali kutibiwa na kuacha miti shamba. Fedha iliyoongezwa haikutosha kununua vifaa vya hospitali na pia haikutosha kupanua shule za kufundishia waganga. Licha ya fedha, hawakuwapo watu wa kutosha wenye elimu iliyotakiwa ili wachukue mafunzo mbali mbali ya uganga. Kazi za utibabu hazikuweza kuendelea pasipo Waafrika wenyewe kupewa ujuzi na madaraka katika kila daraja la wauguzi. Manesi na madaktari Waafrika wengi walitakiwa.

Katika mwaka 1951 halmashauri ya mafunzo ya waganga ilianzishwa. Mafunzo ya miaka mitatu ya wasaidizi wa madaktari yaliendelea Dar es Salaam wakiwa wanachukuliwa wanafunzi waliohitimu darasa la kumi. Mafunzo ya miaka miwili kwa wasaidizi wa madaktari katika hospitali za shamba, yaliendelea Mwanza. Kwa shule ya Mwanza walichukuliwa wanafunzi waliohitimu darasa la nane.

Lakini kwa upande wa kuzuia magonjwa maendeleo hayakuwa makubwa. Mahitaji ya kuwapo** kwa vituo vya kutolea dawa na kuzuia magonjwa katika sehemu za shamba na pia kwa ajili ya kutolea elimu ya mambo ya usafi na afya nzuri yalikuwa makubwa sana. Vituo hivyo vingalikuwa vinatoa dawa na kuwa na vyumba vidogo vya kulaza wagonjwa, vyumba vya kuzalishia na sehemu za kuangalia afya ya watoto wachanga, na pia vyumba vya kutolea mafunzo ya elimu ya usafi na afya. Ilitazamiwa kuwa hatimaye vituo hivyo vingelikuwa badala ya hospitali ndogo.

Katika mwaka 1960 hospitali kubwa ilifunguliwa mjini Dar es Salaam, yaani hospitali iitwayo Muhimbili sasa. Palikuwa pia na hospitali arobaini na nane nyingine za serikali, hospitali kwa matibabu maalumu sita na hospitali ndogo ishirini.

Toka wananchi waanze kushika madaraka ya serikali mwaka 1960 jambo la ubaguzi kwa wagonjwa lilianza kuondolewa pole pole. Hata uhuru ulipofika hapakuwa na hospitali za Wazungu tena. Hospitali zilianza kutibu watu wa rangi yo yote kama ilivyotaka sheria ya serikali. Kwa mfano, hospitali ya ‘Ocean Road’ mjini Dar es Salaam ilianza kuitwa hivyo baada ya kukomesha ubaguzi huo. Zamani ilikuwa inaitwa hospitali ya Wazungu.

Wananchi wengi watumishi wa serikali walipata vyeo vya madaraka makubwa katika Idara ya utibabu toka juu mpaka chini na toka Dar es Salaam mpaka katika miji midogo mingine iliyoko bara. Mipango ya baadaye iliendelea kutegemea kuwapo** kwa fedha na wataalamu, wananchi wengi walizidi kwenda nchi za ng’ambo kujifunza mambo ya utabibu wa aina mbali mbali. Na misheni zilizidi kushirikiana na serikali bega kwa bega katika kuyapiga vita maradhi. Wananchi pia walizidi kutambua faida ya hospitali na walianza kujitolea kujenga majumba ambayo walitaka yatumike kama hospitali katika vita ya kupigana na maradhi.

Wakati huo ulikuwa muda wa jitihada nyingi za kufanya jambo lo lote la kuinufaisha nchi yetu kwa kadiri inavyowezekana. Tanganyika mpya ilihitaji kila raia aone kuwa ana wajibu na yu sehemu ya wajenzi wa taifa jipya.


Maelezo

*…akiwa yungali hai можно перевести как “…еще при жизни…” (буквально: “…будучи еще живым”). Это аналитическая глагольная форма, где -ki- во вспомогательном глаголе -wa показывает, что действие происходит одновременно с другим, основным действием в предложении (aliambatana). Место смыслового глагола в этой конструкции занимает недостаточный глагол -ngali со значением “еще/ все еще/ пока”. Форма yungali может иметь свой вариант angali (но только для 3-го лица ед. числа). Другие примеры:

Mtoto huyu afundishwe lugha yake ya jadi akiwa yungali mdogo “Этого ребенка следует обучать родному языку, пока он еще маленький”;

Afadhali ukile chakula hiki kikiwa kingali moto “Лучше съешь эту еду, пока она еще горячая”.


** В языке суахили нет самостоятельных глаголов со значением “находиться”, “пребывать”, “иметься”, их роль выполняет глагол -wa с локативными формантами. В тексте встретилась инфинитивная форма такой конструкции – kuwapo, выступающая в функции существительного со значением “нахождение”, “пребывание”, “наличие”, “присутствие”. Другие примеры:

Kuwapo kwake mkutanoni kuliwashangaza watu wengi “Его присутствие на собрании удивило многих”;

Waziri alisisitiza kuwako kwa matatizo makubwa “Министр подчеркнул наличие серьезных проблем”.

Противоположное значение (ненахождение, отсутствие) передается с помощью отрицательного инфикса инфинитива -to-: kutokuwapo/kutokuwako/kutokuwamo:

Kutokuwako kwa njia nzuri kulisababisha balaa kubwa “Отсутствие хороших дорог вызвало большую беду”.


Mazoezi

3. Дайте русские эквиваленты:

walishambuliwa na magonjwa; dawa za miti shamba; -punguza maumivu; -ponya maradhi; kazi iliyorithiwa; baba aliambatana na mtoto wake; wangependa kudadisi kama ni kweli; juhudi kubwa ilifanywa; walisitawisha mambo ya utibabu wa kisasa; watumishi wa hospitali; ilitambulikana; mipango ya kuweka kinga kwa magonjwa; idara ya utibabu; upanuaji wa kazi; hali ya usafi na kanuni za afya; kazi za kuondoa uchafu; kazi za dawa zilipunguzwa; kutokula chakula cha kutosha; hospitali mbali kwa Wazungu; -panua shule za kufundishia waganga; -pewa ujuzi na madaraka; kila daraja la wauguzi; kwa upande wa kuzuia magonjwa; vyumba vya kulaza wagonjwa; vyumba vya kuzalishia; -pata vyeo vya madaraka makubwa.


4. Дайте эквиваленты на суахили:

использовать средства народной медицины; излечивать опасные болезни; облегчить невыносимую боль; находиться в сопровождении коллег; средство от головной боли; выведывать чьи-либо секреты; делать огромные усилия; методы современной медицины; обучать медперсонал больницы; ставить заслон на пути болезням; применять вакцину; задачи, стоящие перед департаментом; проверять санитарные условия; соблюдать нормы защиты здоровья; работы по борьбе с загрязнением; фармацевтическая промышленность; проблемы недоедания среди бедного населения; полноценное питание; удовлетворять потребности в лекарствах; приобретать оборудование для больниц; учиться на врача; врачи всех категорий; профилактика болезней; покончить с расовой дискриминацией; получить ответственный пост; тесно сотрудничать; объявить войну болезням; приносить пользу народу.


5. Переведите и перескажите следующие тексты:

Hospitali ya Ocean Road

Hospitali maarufu sana iliyopo jijini Dar es Salaam katika barabara ijulikanayo kwa jina la Ocean Road, imetimiza miaka 100. Hospitali hii kwa sasa inahudumia wagonjwa wa kansa.

Sherehe za maadhimisho hayo zilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa utamaduni wa Ujerumani ambapo ilihudhuriwa na waziri wa afya.

Hospitali ya Ocean Road imegeuzwa kuwa hospitali ya kuhudumia wagonjwa wa kansa tangu mwaka 1987. Kabla ya hapo hospitali hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuhudumia majeruhi wa kivita wakati wa ukoloni.

Baada ya Tanzania kupata uhuru, hospitali hiyo iligeuzwa kuwa ya serikali ambapo ilianza kutoa huduma za uzazi zilizohamishwa kutoka hospitali ya Muhimbili.


Chanjo ya homa ya manjano haina haja tena

Wizara ya afya ya Tanzania imefuta sharti la kuonyesha cheti cha chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya manjano kwa wasafiri wanaoingia nchini.

Hapo kabla kumekuwako na utaratibu wa kuhakikisha kuwa kila mgeni anayeingia nchini awe amepata chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya manjano, utaratibu uliokuwa unawahusu hata wageni wanaotoka katika nchi jirani za Kenya na Uganda.

Wizara ya afya imefanya uamuzi wa kuondoa sharti la kuwa na cheti cha chanjo dhidi ya ugonjwa huo kwa wasafiri wote wanaoingia nchini kwa kupitia katika viwanja vya ndege na vituo vya mipakani.

Hata hivyo taarifa ya wizara hiyo imewashauri wasafiri wote kuendelea kupata chanjo hiyo hasa wale ambao watakuwa wanasafiri kwenda au kupita katika nchi zenye ugonjwa wa homa ya manjano kama za Afrika ya Kati, Afrika ya Magharibi na Amerika ya Kusini.


6. Переведите, используя аналитическиее формы в подчеркнутых глаголах:

1. Пребывая в состоянии гнева, начальник уволил своего лучшего сотрудника. 2. Вдалеке я увидела свою подругу, ехавшую на велосипеде. 3. Путешествуя по Танзании, мы видели множество обезьян, пересекающих дорогу со своими детенышами на спине. 4. Войдя в спортивный зал, я увидел своих сокурсников, играющих в баскетбол. 5. Композитор сочинил свою самую популярную песню, будучи еще совсем молодым. 6. Будучи все еще маленьким ребенком, он каждый раз начинал плакать, когда его мама уходила на работу. 7. Они плохо разбирались в этом деле, которое было все еще новым для них. 8. Чувствуя себя все еще больным, он отказался поехать в командировку.


7. Закончите предложения:

1. Ningalikuwa baharia katika meli kubwa … 2. Ningalikuwa waziri wa sheria wa nchi hii … 3. Ningalikuwa inspekta mkuu wa polisi … 4. Laiti ningelikuwa simba katika hifadhi ya wanyama … 5. Kama ningalikuwa mfanya biashara tajiri sana … 6. Ningalikuwa na paka 20 nyumbani mwangu … 7. Kama ningalikuwa na ndege kubwa ya kibinafsi … 8. Ningalikuwa sultani mwenye watumishi wengi … 9. Kama ningalikuwa na watoto kumi … 10. Laiti ningaliishi katika enzi ya wafalme wa Urusi …


8. Сделайте письменный перевод следующих текстов:

Ukimwi

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi Dakta Peter Piot amesema kuwa, Umoja wa Mataifa umeamua kuwa, kuanzia sasa fedha za kutosha zitatengwa kwa ajili ya kupambana na kuenea kwa virusi vya ukimwi katika Bara la Afrika.

Dakta Piot ameyasema hayo, wakati akiwahutubia wanachama wa chama kisichokuwa cha kiserikali cha walio katika mapambano na ukimwi nchini, alipotembelea ofisi ya huduma ya chama hicho jijini Dar es Salaam. Amesema, pamoja na uhakika huo uliotolewa na Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake, bado kuna haja kubwa kwa kila taifa kuchukua hatua za makusudi katika kuhakikisha kuwa ukimwi unapigwa vita na kila mwananchi pale alipo.

Pia amesema ni jambo la kutia moyo kuona kuwa, kasi ya maambukizo ya virusi vya ukimwi, na ukimwi mkoani Mbeya, imepungua katika miaka mitano iliyopita, wakati ambapo Botswana inaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa ukimwi duniani, ikifuatiwa na Afrika Kusini na Zimbabwe wakati dunia nzima ina mamilioni ya wagonjwa wa ukimwi hivi sasa.

Naye mwenyekiti wa chama hicho Profesa Kanywanyi amesema, inawezekana kujikinga kuambukizwa virusi vya ukimwi kwa kutoa elimu, ushauri pamoja na kuimarisha mawasiliano dhidi ya ukimwi na virusi vyake, kwa kupashana habari katika jamii kuhusu ugonjwa huo wa hatari.